Friday, 24 February 2017

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI AAGIZA KUKAMATWA MWENYEKITI WA MTAA WA KIJITONYAMA

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni ameagiza kukamatwa kwa mwenyekiti Philipo Komanya wa mtaa wa Kijitonyama baada ya kutuhumiwa kuhujumu mali za kata wa mtaa wa huo .
Mwenyekiti huyo alifungua akaunti mbili, ikiwa moja ya  kwake  nyingine ya serikali ya mtaa  na alikuwa anatumia zaidi ya kwake kwa mali za wananchi, Licha ya kufungua akaunti hizo bado alikusanya 54,000 kwa ajiri ya mfereji ambapo hakuweza kutekeleza kuukarabati mara baada ya kupata pesa hizo.
 Katika hatua nyingine  kata hiyo imegundua maeneo 25 ya wazi ambayo yalikuwa yanatumiwa na watu binafsi, baada ya kugundua hilo  viongozi wa kata wameweza kukusanya mapato shilingi milioni 57 katika maeneo  17 , huku yakibakia maeneo 8 ambayo yanafanyiwa kazi ili kukusanya mapato hayo.
Hapi ameagiza kuletwa kwa meneja katika soko la Mwenge ili kudhibiti mapato ambayo yanapotea kwa wakusanyaji waliopo sasa. Pia ameagiza Manispaa kupata shilingi 500 kwa kila kichwa kinachofanya kazi katika soko hilo . Amewaomba wananchi kuacha tabia ya kuripoti matatizo yao  kwa viongozi wa juu badala yake wafuate utaratibu uliosahihi na satasaidiwa matatizo yao.

No comments:
Write comments