Monday 20 March 2017

MAGUFULI ATUPIA KAPUNI ISHU YA MAKONDA,......ATUMA DONGO ZITO KWA WANAOMPOST VIBAYA


Image result for magufuliRais Magufuli: "Tumejielekeza mno katika masuala ya udaku ambayo hayatuongezei chochote, hayatusaidii chochote na ndio yanachukua muda wetu mwingi. Tuzungumze uchumi, tujielekeze katika mambo ya maendeleo na hayana chama na nafurahi kumuona mstahiki meya na ni wa CHADEMA.

Kampeni zilishakwisha, ulie ugalegale Rais ni Magufuli. Ndio maana hii interchange inajengwa kwenye jimbo la CHADEMA, nawaomba watanzania wa vyama vyote tujifocus kwenye suala la maendeleo.

Mnahangaika mnapost kwenye vipost vyenu, mpaka watu wengine wanaingilia uhuru wangu, mimi huwa sipangiwi mambo. Mimi ni Rais ninayejiamini, siwezi kupangiwa, hata siku ya kuchukua fomu nilienda mwenyewe.

Nitaamua mwenyewe nani akae wapi, kwa hio Makonda wewe chapa kazi, nasema chapa kazi. Najua wamenielewa, kuandikwa kwenye mitandao sio tija kwangu, hata mimi naandikwa kwenye mitandao, Kwahio nijiuzulu Uraisi?

Mimi ningefurahi hata kwenye mitandao tungekuwa tunapata ushauri jinsi ya kufanya kazi, tunajadili personality na sio ideas, tuchape kazi kwa manufaa ya watanzania.







No comments:
Write comments