Monday 20 March 2017

Baada ya maelezo ya Gwajima na Ruge, haya hapa makosa matano(5) mazito ambayo ndiyo kichinjio tosha cha kumchinja Makonda

Image result for funga pingu na polisi
Baada ya kusikia maelezo ya Askofu Gwajima, na Ruge Mutahaba; yakithibitika Ofisi ya Mwendesha mashtaka wa Serikali wanayo mashitaka ya wazi ambayo yanaushahidi usio na shaka dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambayo ni:

1. Unyang'anyi wa kutumia silaha (armed robbery) kinyume na kifungu 287A cha Sheria ya Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 ya sheria zetu.

2. Matumizi mabaya ya ofisi (abuse of office) kinyume na kifungu 96(1) cha Sheria ya Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 ya sheria zetu.

3. Matumizi mabaya ya wadhifa (abuse of position) kinyume na kifugu cha 31 cha Sheria ya Kupambana na kuthibiti Rushwa ya mwaka 2007

4. Kuingia kijinai (Forcebly Entry) kinyume na kifungu 85 cha Sheria ya Kanuni za Adhabu sura ya 16 ya sheria zetu.

5. Kutishia kwa lengo la kulazimisha (intimidation) kinyume na kifugu 89B cha Sheria ya Kanuni za Adhabu sura ya 16 ya Sheria zetu. shtaka la kwanza halina kabisa dhamana.

Kama ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka haikumuogopa marehemu Ukiwaona Ditopile Mzuzuri (aliekua mkuu wa mkoa wa Tabora wakati huo, na mshenga wa Rais Kikwete) na kumshitaki kwa mauaji, kitu gani leo kinawafanya msimpeleke Mahakamani huyu Mkuu wa Mkoa wa Dar ambae wala sio mshenga wa Rais? 
ℹjhnmallya2017

No comments:
Write comments