WIKIENDI
hii Mashabiki wa Soka la England watashuhudia Mechi mchanganyiko za
EPL, Ligi Kuu England, na zile za EMIRATES FA CUP ambayo ipo Robo
Fainali.
Jumamosi zipo Mechi 3 za EPL na 2 za FA CUP.
Kwenye
Ligi, Bournemouth, ambao Wiki iliyopita waliibana Man United na kupata
Sare 1-1 huko Old Trafford lakini Beki wao Tyrone Mings akafungiwa Mechi
5, wapo Nyumabani kuivaa West Ham.
Mechi nyingine za Ligi ni Everton na West Brom na ile ya Hull City na Swansea City.
Kwenye
FA CUP hiyo Jumamosi ni Middlesbrough na Man City huko Riverside wakati
Arsenal ikiwa kwao Emirates Jijini London kucheza na Timu isiyokuwa
kwenye Mfumo rasmi wa Ligi Lincoln City.
Jumapili
EPL ina Mechi tu huko Anfield kati ya Liverpool na Burnley na FA CUP
itachezwa huko White Hart Lane kati ya Tottenham na Millwall.
Jumatatu
Usiku Mechi pekee ni mtange mkali wa FA CUP huko Stamford Bridge kati
ya Wenyeji Chelsea na Mabingwa Watetezi wa Kombe hilo Man United.
EPL, LIGI KUU ENGLAND
Ratiba
Jumamosi Machi 11
1800 Bournemouth v West Ham United
1800 Everton v West Bromwich Albion
1800 Hull City v Swansea City
Jumapili Machi 12
1900 Liverpool v Burnley
FA CUP
Ratiba
Raundi ya 6 [Robo Fainali]
**Saa za Bongo
Jumamosi Machi 11
1515 Middlesbrough v Man City
2030 Arsenal v Lincoln City
Jumapili Machi 12
1700 Tottenham Hotspur v Millwall
Jumatatu Machi 13
2245 Chelsea v Manchester United
Saturday 11 March 2017
EPL YAENDELEA WIKIEND HII VIGOGO WAPO FA CUP
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Write comments