Monday 13 March 2017

Maporomoko ya takataka yaua zaidi ya watu 30 Ethiopia

Maporomoko ya taka yaua watu 15 Ethiopia

Zaidi ya watu 30 wameuawa na maporomoko ya taka kwenye eneo moja kubwa la kumwaga taka nje ya mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.
Inaripotiwa kuwa watu kadha bado hawajulikani waliko tangu maporomoko hayo yatokee siku ya Jumamosi usiku.
Inaaminiwa kuwa watu takriban 150 walikuwa eneo hilo.
Mabanda kadha ya watu kwa sasa yamefukiwa chini ya tani kadha za taka.
Eneo hilo limekuwa likitumiwa kutupa taka kutoka kote mjini Addis Ababa kwa zaidi ya miongo mitano.
Maporomoko ya taka yaua watu 15 Ethiopia

Watu wengi wamekuwa wakisaka eneo hilo kujitafutia riziki huku wengine wakiwa ni wenyeji .
Serikali nayo imekuwa ikijenga kiwanda kwa kwanza kabisa barani Afrika, kwa lengo ya kuibadili taka hiyo kuwa nishati karibu na eneo hilo.
Wana mpango ya kuchoma taka kutoka mjni Addis Ababa na kuugeuza kuwa umeme

No comments:
Write comments