Friday 31 March 2017

Mikataba 15 imesainiwa Ikulu leo March 31, 2017


7-7
Waziri Mkuu wa Ethiopia HAILEMARIAMU DESALEGN amewasili leo nchini na kupokelewa na mwenyeji wake rais John Pombe Magufuli, wakiwa Ikulu jijini dar es salaam pamoja na mazungumzo ya faragha, pia wamesaini mikataba 15 ambayo inalenga kukuza uchumi wa nchi hizo mbili.
Miongoni mwa mikataba iliyosainiwa na Waziri Mkuu huyo wa Ethiopia ni pamoja na ule wa Ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Ethiopia wenye lengo la kupambana na wahamiaji haramu,Ushirikiano kwenye sekta ya usafiri wa anga, utalii, viwanda hasa vya ngozi na nyama, umeme pamoja na masuala ya kilimo.
Wakizungumza mara baada ya utiaji saini mikataba hiyo iliyosainiwa na mawaziri wenye dhamana kutoka nchi zote mbili,
Rais John Magufuli na waziri mkuu wa Ethiopia wamesema ushirikiano kati ya nchi hizo mbili inalenga kunufaisha nchi zote mbili kiuchumi, ambapo pia Ethiopia imekubali kufungua ubalozi wke hapa nchini.
Mambo mengine yaliyoongelewa kwenye mkutano wao wa ndani ni pamoja na matumizi ya maji ya mto Nile, na hapa rais Magufuli anafafanua.
Rais Magufuli amempongeza waziri mkuu wa Ethiopia kwa kuonyesha nia ya dhati ya kukuza kiswahili kwenye nchi yake ambapo wataanza kufundisha kwenye baadhi ya vyuo vikuu.
Waziri mkuu wa Ethiopia yupo nchini kwa ziara ya siku mbili ambapo kabla ya kuanza safari ya kurudi nchini mwake, atatembelea bandari ya Dar es salaam ili kujionea namna wanavyoweza kuitumia bandari hiyo kusafirishia mizigo, kwa ushirikiano na shirika la ndege la Ethiopia.

No comments:
Write comments