Msukuma : Sioni tatizo kwa Nape kuoneshwa bastola
Akihojiwa
jana, Msukuma alidai kwa walichokifanya watu wanaodaiwa ni askari
kumuonyesha bastola Nape ni sahihi kwani kitambulisho cha askari yeyote
ni bastola au bunduki hivyo Nape hakupaswa kuwa na shaka maana walikuwa
wanamlinda. Msukuma alikwenda mbali zaidi na kusema hata yeye
alionyeshwa SMG nane lakini hakuwa na shaka maana wale ni askari.
Aidha Msukuma alisema kuwa Nape alipaswa kutulia kwanza hata kwa miezi mitatau ndipo angezungumza aliyotaka kuzungumza.
Pia amemsihi Nape kuacha hasira mara
baada ya kutenguliwa kuwa waziri kwani wakati anaomba kura katika jimbo
lake la Mtama hakuomba na uwaziri, hivyo asilie kuenguliwa katika
wadhifa huo kwani bunge lina wabunge 360 na kila mbunge angependa kuwa
waziri, hivyo kuenguliwa kwake katika nafasi hiyo inawapa nafasi wabunge
wengine nao kuwa mawaziri siku moja na hata yeye anatamani kuwa waziri.
No comments:
Write comments