Wakati Mkutano Mkuu wa Chama cha
Mapinduzi (CCM) ulipokuwa ukiendelea mkoani Dodoma, baadhi ya waliokuwa
wanachama na viongozi wa ngazi za juu wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) pamoja na ACT-Wazalendo wamepokelewa rasmi na CCM
baada ya kutangaza kujiunga na chama hicho.
Viongozi hao waliojiunga na CCM juzi wamesema sababu kubwa iliyopelekea na kufikia uamuzi huo ni utendaji
kazi wa Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dkt John Pombe Magufuli.
Miongoni mwa wengi waliopokelewa juzi ni
pamoja na, Moses Machali Mbunge wa zamani wa Kasulu Mjini kwa tiketi ya
NCCR- Mageuzi na baadae kuahimia ACT Wazalendo. Alitangaza kujiunga CCM
Novemba mwaka jana ambapo jana amepokelewa rasmi. Dkt Yared Fubusa,
Aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Mkoa wa Kigoma na Mgombea
Ubunge jimbo Kigoma Kaskazini (CHADEMA).
Mwingine aliyetangaza kujiunga na CCM
na kupokelewa na Mkutano Mkuu ni, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa
CHADEMA Taifa, Said Arfi
No comments:
Write comments