Friday, 24 February 2017

UPNDE WA PILI WA JOKATE

AMINI NYAUNGO
Mwanamuziki na mjasiliamali Jokate Mwegelo ama maarufu kama Kidoti sasa amejaribu kufungua njia katika michezo, alianza kufungua kiwanja Shule ya Sekondari Jangwani ambacho mahususi kwa Netball, hii haikuwa kimakosa bali amedhamiria kuendana na michezo kwani upande wa michezo hauko sawa.
Katika harakati hizo Jokate ameweza kukutana na mastaa mbalimbali Marekani na kupiga nao picha huku akisema  ”Tupo katika majadiliano leo juu ya jukumu la wanariadha na watumbuizaji ya kuwa mfano wa kuigwa na kujenga njia ya kizazi kijacho cha Waafrika” ameandika hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Hii ni dhahiri kabisa kuwa licha ya kufuatilia mambo yake ya kimaisha lakini ana tumaini la wazi kabisa kwa ajili ya kulivusha soko letu la michezo na muziki mbele zaidi.
Kiongozi anaweza kuangaliwa kwa namna nyingi moja wapo muangalie namna anavyohangaika kwa ajili ya wenzake , pili angalia namana gani anajishughulisha, pongezi kwa wote wanaojitolea kwa ajili ya wenzao

No comments:
Write comments