Monday 27 March 2017

BREAKING NEWS:WAZIRI AAGIZA NAY WA MITEGO AACHILIWE


Ney wa Mitego alikamatwa kuhusiana na wimbo wake alioutoa hivi karibuni

Waziri wa Habari nchini Tanzania Dkt Harrison Mwakyembe ameagiza msanii aliyekamatwa kuhusiana na wimbo wake alioutoa hivi karibuni aachiliwe huru.

Sehemu ya maudhui ya wimbo huo inagusia tuhuma za kughushi vyeti ambazo zimekuwa zikigonga vichwa vya habari nchini Tanzania

Mwanamuziki Ney wa Mitego akamatwa Tanzania

Magufuli ayaonya magazeti Tanzania

Nay wa Mitego hata hivyo ametakiwa auboreshe zaidi wimbo wake, kwa mujibu wa ujumbe uliopakiwa katika ukurasa Rasmi wa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania kwenye Twitter.

Wimbo huo mpya wa Ney wa Mitego, ulianza kusambaa katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Ulrich Matei alikuwa amesema mwanamuziki huyo alikamatwa kwa kosa la kutoa wimbo wenye maneno ya kashfa dhidi ya serikali

No comments:
Write comments