Wednesday 22 March 2017

Maamuzi ya Vyombo vya Habari kuhusu sakata la Rc Makonda


Kinachoendelea kuzungumzwa kila pembe ya nchi ni juu ya tukio la hivi karibuni la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kuvamia kituo cha Clouds redio na televisheni akiwa na askari wenye silaha akilazimisha kipindi kinachomhusu Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima na mama anayedaiwa kuzaa nae kisha kumtelekeza kirushwe hewani.

Kitendo hicho kimeibua hisia za wengi huku wadau wa habari na watu wa kada mbalimbali wakilaani vikali kwa vile alichokifanya Rc Makonda ni kosa la jinai na kuingilia uhuru wa vyombo vya habari.
Sasa leo Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) pamoja na Klabu ya Waandishi wa Habari Dar es Salaam (DCPC) kwa pamoja wametoa tamko.

No comments:
Write comments