Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda leo amefika mbele ya
kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kufuatia wito wa Kamati hiyo
kumtaka afike mbele ya kamati kujibu tuhuma zinazomkabili za kuingilia
Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge kutokana na matashi aliyoyatoa mapema
mwezi februari 2017 jijini Dar es Salaam yaliyokuwa na madai ya kudharau
Bunge.
Wito wa kufika mbele ya Kamati hiyo unafuatia Azimio la Bunge lilitolewa
tarehe 8 Februari 2017 ambapo Bunge liliazimia Mhe. Spika aweze
kukubali Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Alexandra Mnyeti na Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam Mhe. Mhe Paul Makonda wahojiwe kutokana na Matamshi
yao ya Kudharau Bunge.
No comments:
Write comments