Tuesday 7 March 2017

Vannesa Mdee Akamatawa kwa Amri ya Makonda

Jeshi la Polisi Dar es Salaam limemshikilia Mwanamziki Vennesa Mdee maarufu kama Vee Money kwa tuhuma za kujihusisha na dawa za kulevya.
Mwanasheria wake Aman Tenga ametihibitisha kuwa mteja wake amejisalimisha mwenyewe Kituo Kikuu cha Polisi, kama ilivyoagizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda wakati akitaja majina ya wanaojihusisha mwezi uliopita.
Mwanasheria Tenga pia ametihibitisha kuwa Vanessa alikuwa Afrika Kusini kikazi wakati jina lake likitajwa na Mkuu wa Mkoa. Pia aliongeza Polisi walikwenda Nyumbani kwa Vanessa kufanya upekuzi kabla ya kumpeleka kwa Mkemia Mkuu wa serikali kwa uchunguzi zaidi.
Mtanzania wa kwanza kuwa mtangazaji wa MTV VJ, Mdee, alizaliwa mwaka 1988 Arusha, alianza kufahamika zaidi mara baada ya kutangaza kwenye Redio na Luninga kwenye vipindi kama Epic Bongo Star Search na Dume Challenge na baadae kidogo wakati ananza alikuwa chini ya Lebo B’hitts

No comments:
Write comments