Jeshi
la Polisi Dar es Salaam limemshikilia Mwanamziki Vennesa Mdee maarufu
kama Vee Money kwa tuhuma za kujihusisha na dawa za kulevya.
Mwanasheria
wake Aman Tenga ametihibitisha kuwa mteja wake amejisalimisha mwenyewe
Kituo Kikuu cha Polisi, kama ilivyoagizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam Paul Makonda wakati akitaja majina ya wanaojihusisha mwezi
uliopita.
Mwanasheria Tenga pia
ametihibitisha kuwa Vanessa alikuwa Afrika Kusini kikazi wakati jina
lake likitajwa na Mkuu wa Mkoa. Pia aliongeza Polisi walikwenda Nyumbani
kwa Vanessa kufanya upekuzi kabla ya kumpeleka kwa Mkemia Mkuu wa
serikali kwa uchunguzi zaidi.
Mtanzania
wa kwanza kuwa mtangazaji wa MTV VJ, Mdee, alizaliwa mwaka 1988 Arusha,
alianza kufahamika zaidi mara baada ya kutangaza kwenye Redio na
Luninga kwenye vipindi kama Epic Bongo Star Search na Dume Challenge na
baadae kidogo wakati ananza alikuwa chini ya Lebo B’hitts
No comments:
Write comments