Sunday 2 April 2017

Uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Katavi, Serikali yasema imeandaa mkakati kujenga uchumi wa viwanda



Serikali kupitia wizara ya viwanda ,biashara na uwekezaji imeandaa mkakati wa kujenga uchumi wa viwanda unaohusisha sekta zote za uchumi katika kipindi cha miaka mitano 2015 – 2020 lengo likiwa kutekeleza azma yake ya kuchochea uchumi wa viwanda ili nchi kufikia uchumi wa kati.

Hayo yamesemwa na makamu wa pili wa rais wa Zanzibar balozi Self Ally Iddy katika uzinduzi wa mbio za mwenge kitaifa mkoani katavi yenye kauli mbiu ya mwaka huu shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu.

Kwa upande wao waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera, bunge , vijana, ajira, bunge na walemavu Jenista Mhagama na Waziri wa kazi, uwezeshashi , vijana, wazee, wanawake na watoto Zanzibar Maudlin Cyrus Castico amese.

Mkuu wa mkoa wa katavi meja jenerali mstaafu Raphael Muhuga amesema kuwa mwenge wa uhuru utazindua miradi mbalimbali katika mkoa wa katavi.

No comments:
Write comments