Friday 31 March 2017

Safari maalumu ya Treni Dar-Burundi yazinduliwa


Kampuni ya Reli Tanzania imezindua rasmi huduma maalumu ya usafirishaji wa shehena kwa njia ya reli kutoka dar es salaam kwenda Burundi kwa kutumia train nzima(Block Train).
Akizungumza muda mfupi kabla ya kuanza safari kwa treni hiyo , kaimu mkurugenzi mtendaji TRL Shaban Kiko amesema treni hiyo yenye mabehewa 20 ambazo zina uwezo wa kubeba tani 40 kila behewa, imebeba mzigo wa malighafi ya chuma ambao utasafirishwa kwa siku tatu hadi kuingia mkoani kigoma na siku moja kuwasili mjini Bujumbura Burundi.
Kwa mujibu wa TRL imepunguza gharama za usafirishaji wa mizigo ya kawaida na ile inayohifadhiwa katika makasha kwenda Burundi ambapo hivi sasa inatoza kiasi cha dola 3,056 kwa behewa moja la mizigo ya kawaida na dola 3024 kwa mizigo iliyofungwa kwenye makasha ikilinganishwa na gharama zinazotozwa kwa njia ya barabara ambazo ni dola 3500.

No comments:
Write comments