Monday 5 June 2017

SAKATA LA GWAJIMA,BASHITE LAIBUKA UPYA

Image result for GWAJIMA

Jana katika kanisa la Ufufuo na Uzima Yule askofu machachari Askofu Gwajima amejibu mashambulizi ya hotuba ya RC wa Dar Es Salaam yaliyofanyika television ya Star TV majuma kadhaa yaliyopita. Amechambua hotuba yote aliyofanya RC pale Star TV, ameeleza elimu ya Nape Nnauye, amechambua tukio la uvamizi pale Clouds FM na akaeleze uhalali wa jina la Bashite Kwa RC. Askofu Gwajima ameshusha nondo zake za kutosha kudhihirisha kuwa muhusika wa hotuba jina lake halali ni Bashite. Ameenda mbali na kudai kuwa hata namba za simu za baba yake kwenye miamala ya fedha zimesajiliwa kwa jina la Bashite. Na akaitaja namba husika. Anasema kabla sakata halijapamba moto bila wao kushtukia aliruka had mwanza na ana picha alizopiga kwenye rejesta za shule ya msingi na sekondari na majina ya muhusika yalikuwa ni Bashite. Pia askofu Gwajima anasema wiki iliyopita aliwasiliana na Anthony Diallo kumuuliza kwa nin aliruhusu kipindi cha kumdhalilisha. Askofu anasema Mh Diallo alimjibu kuwa aliweza kumruhusu kumpa kipindi kwa kuwa Bashite alimuambia kuwa nataka kuonyesha vyeti kwa watanzania na hivyo Diallo akaona ni jambo jema. Askofu anasema hata baada ya kipindi Mh Diallo alishangaa kwa sababu Bashite hakufanya kama alivyoomba. Askofu akaonyesha ujumbe mfupi wa simu uliotoka kwa Diallo.

No comments:
Write comments