Friday 21 July 2017

NIONZIMA AMALIZA MKATABA WAKE YANGA SASA RASMI AELEKEA HUKU



Image result for nionzima 
Kwa kuwa kiungo Haruna Niyonzima, rasmi amemaliza mkataba wake na Yanga, Simba iko huru kumtambulisha wakati wowote ule.

Simba imemsajili Niyonzima raia wa Rwanda lakini imekuwa ikificha mambo kwa hofu ya kuonekana imemsajili mchezaji huyo kabla mkataba kwisha.

Baada ya mkataba wake kwisha maana yake, Simba inaweza kumtangaza Niyonzima kuanzia leo, kesho au keshokutwa na baada ya hapo itakuwa huru kuendelea na shughuli zake.

Simba ilimsajili Niyonzima baada ya Yanga kushindwa kumalizana naye na kumpa ruhusa kuendelea na kusaka timu kokote anakotaka.


Mnyarwanda huyo ameichezea Yanga kwa mafanikio makubwa huku akiwa ni injini ya uchezeshaji.

No comments:
Write comments