Kuna
taarifa kwamba kuwa kusaini kwa kiraka, Erasto Nyoni Simba kumevuruga
mipango ya Kocha Mkuu wa Yanga, Mzambia, George Lwandamina kwenye kikosi
chake.
Kiraka huyo, inaelezwa aliingia makubaliano ya kusaini mkataba wa miaka miwili Simba pamoja na Said Mohamed 'Nduda'.
Awali, kiraka huyo ilielezwa kufikia makubaliano mazuri na Yanga kwa ajili ya kusaini mkataba wa kuichezea timu hiyo.
Kwa
mujibu wa mtoa taarifa kutoka ndani ya Yanga, Kocha Lwandamina ndiye
aliyetoa mapendekezo ya usajili wa mchezaji kiraka atakayemudu kucheza
nafasi zaidi ya moja kwenye kikosi chake.
Mtoa
taarifa huyo alisema walifikia makubaliano mazuri na kiraka huyo kwa
asilimia 50, lakini wakashangazwa na taarifa za kusaini Simba mkataba wa
miaka miwili.
"Tukiri
ni kweli kabisa Nyoni tulikuwa naye kwenye mipango mizuri na mazungumzo
yetu yalikuwa mazuri, hivyo tulishangaa kusikia amesaini Simba.
“Kikubwa
kocha ndiye alikuwa anaomba asajiliwe mchezaji mmoja kiraka mwenye
uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja, kwa maana siku akitokea mchezaji
mmoja majeruhi au mwenye adhabu ya kadi, basi yeye anaziba nafasi yake,”
alisema mtoa taarifa huyo.
Kauli
hiyo ilithibitishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga,
Hussein Nyika bila ya kumtaja mchezaji huyo, akisema: “Katika usajili
wetu, kuna wachezaji tuliokuwa nao kwenye mipango ya kuwasajili, lakini
tumewakosa, hivyo tunatafuta wengine wenye uwezo.”
No comments:
Write comments