Friday 21 July 2017

SIMBA WAWAPIGA WAPINZANI WAO GOLI LA MWAKA,YANGA WALALAMA MCHEZAJI MPYA WA SIMBA ALIVYO WAVURUGA.



Kuna taarifa kwamba kuwa kusaini kwa kiraka, Erasto Nyoni Simba kumevuruga mipango ya Kocha Mkuu wa Yanga, Mzambia, George Lwandamina kwenye kikosi chake.

Kiraka huyo, inaelezwa aliingia makubaliano ya kusaini mkataba wa miaka miwili Simba pamoja na Said Mohamed 'Nduda'.

Awali, kiraka huyo ilielezwa kufikia makubaliano mazuri na Yanga kwa ajili ya kusaini mkataba wa kuichezea timu hiyo.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa kutoka ndani ya Yanga, Kocha Lwandamina ndiye aliyetoa mapendekezo ya usajili wa mchezaji kiraka atakayemudu kucheza nafasi zaidi ya moja kwenye kikosi chake.

Mtoa taarifa huyo alisema walifikia makubaliano mazuri na kiraka huyo kwa asilimia 50, lakini wakashangazwa na taarifa za kusaini Simba mkataba wa miaka miwili.

"Tukiri ni kweli kabisa Nyoni tulikuwa naye kwenye mipango mizuri na mazungumzo yetu yalikuwa mazuri, hivyo tulishangaa kusikia amesaini Simba.

“Kikubwa kocha ndiye alikuwa anaomba asajiliwe mchezaji mmoja kiraka mwenye uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja, kwa maana siku akitokea mchezaji mmoja majeruhi au mwenye adhabu ya kadi, basi yeye anaziba nafasi yake,” alisema mtoa taarifa huyo.

Kauli hiyo ilithibitishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Hussein Nyika bila ya kumtaja mchezaji huyo, akisema: “Katika usajili wetu, kuna wachezaji tuliokuwa nao kwenye mipango ya kuwasajili, lakini tumewakosa, hivyo tunatafuta wengine wenye uwezo.”

No comments:
Write comments