Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar
es salaam limefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi milioni 840 za faini
ya makosa mbalimbali ya barabarani kwa kipindi cha wiki moja ya
oparesheni iliyofanywa na jeshi hilo.
Akiongea na waandishi wa habari Ijumaa
hii, Kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema
kiwango cha mapato hayo ni kidogo na inaashiria kupungua kwa makosa
yanayofanywa na madereva.
“Kwa upande wa barabarani tunakwenda
vizuri kati ya tarehe 1 mwezi 3 mwaka 2017 mpaka tarehe 9 mwezi wa 3
mwaka 2017 takribani siku hizo 8 tumeweza kukusanya jumla ya shilingi
milioni 840 kwahiyo niseme tu kwamba mapato yanapungua hii tu ni
kwasababu watu wameanza kutii tu sheria ya usalama barabarani,” Alisema
Kamanda Sirro
No comments:
Write comments