Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Yusuf Masauni, ameagiza
kupanguliwa kwa maofisa wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya wa
Idara ya Polisi na Uhamiaji waliopo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Abeid Aman Karume mjini Unguja.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mara baada ya Masauni
kutembelea uwanja huo na Bandari kuu ya Zanzibar, ilisema kuwa baadhi ya
maofisa wamekuwa na tabia ya kuzima mashine za ukaguzi wa mizigo kwa
makusudi ili kupitisha vitu haramu zikiwamo dawa za kulevya.
“Ingawa polisi wana kitengo maalumu cha kupambana na dawa hizi, lakini
bado tatizo hili linazidi kushamiri hapa Zanzibar,” alisema Mhandisi
Masauni katika taarifa hiyo.
Pia, naibu waziri huyo ameagiza wafanyakazi wa idara ya uhamiaji na
polisi waliofanya kazi katika eneo moja kwa zaidi ya miaka miwili
kuhamishiwa kwenye vituo vingine ili kusaidia kudhibiti uingizwaji wa
dawa za kulevya visiwani humo.
Katika ziara hiyo, Mhandisi Masauni aliambatana na Naibu Waziri wa
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Mohamed Ahmada Salum.
Mkuu wa idara ya uhamiaji uwanjani hapo, Kamishna Msaidizi Fulgence
Mutarasha alisema katika vita ya kupambana na dawa hizo mwaka jana
waliwakamata abiria 29 na kuwaweka chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi
kwa uchunguzi zaidi
Friday 10 March 2017
KUMEKUCHA ZANZIBAR KASI YA MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA YA HAMIA VISIWANI HUKO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Write comments