Baadhi ya wagombea wa nafasi ya
urais kupitia kwa chama cha wanasheria wa Tanganyika TLS wanatarajia
kuwasilisha maombi ya kujumuishwa kama wadaiwa katika kesi ya kupinga
kufanyika kwa uchaguzi wao uliopangwa kufanyika tarehe 18 ya mwezi huu.
Wamefikia hatua hiyo ili kuuongezea nguvu
upande wa wadaiwa kufuatia kesi iliyofunguliwa na wanachama wawili wa
chama hicho ambao wamefungua kesi katika mahakama kuu kupitia mkoa wa
Dodoma na Dar es salaamu .
Wakizungumza na waandishi wa habari jijini
Dar es salaam mgombea TUNDU LISSU amesema uchaguzi huo umekuwa
ukifuatiliwa kwa karibu na watu wengi huku akibainisha kuwa kuna kile
alichokiita njama dhidi ya kuuharibu uchaguzi huo
Lissu ameongeza kuwa wanachama wa chama
hicho hawatakuwa tayari kuona uchaguzi unasitishwa kutokana na sheria za
chama hicho kusisitiza kufanyika kwa uchaguzi wa chama hicho ambacho
amedai kimekuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya sheria nchini.
Katika kesi ya msingi ya kupinga uchaguzi
huo iliyofunguliwa na wanachama hao, washtakiwa ni mwanasheria mkuu wa
serikali pamoja na chama chenyewe (TLS).
Kwa upande wake mgombea mwingine wa nafasi
ya urais ambaye aliwahi kuwa waziri wa mambo ya ndani mheshimiwa
LAWRENCE MASHA amebainisha kuwa chama chao hakina kipengele chochote
kinachozuia wanasiasa kugombea nafasi ya uongozi katika chama hicho huku
akiwataka wanachama wa chama hicho kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano
mkuu wa chama hicho ambao unatarajiwa kufanyika mkaoni Arusha siku ya
tarehe 18 ya mwezi huu
No comments:
Write comments