Rais wa Jamhuri wa Muungano wa
Tanzania siku ya leo amemjibu maombi ya moja kwa moja juu ya kilio cha
wasanii kilichowakilishwa na msanii Diamond Platnumz.
Akizungumza moja kwa moja kutoka Ikulu
Rais Magufuli kupitia Simu aliyoipiga kipindi cha Clouds 360, Rais
alimueleza Diamond kuwa maombi yake ameyasikia na atayafanyia kazi kwa
ukaribu.
Aidha Rais Magufuli amempongeza Diamond
kwa moyo wake wa kujituma na kazi nzuri anazofanya kwa jamii pia
amefurahishwa na msanii huyo kupata watoto wawili kwasasa kwani kipindi
cha kampeni alikuwa na mtoto mmoja
kilichomeweka gumzo ni pale Rais Magufuli
alipogusia kuwa anavutiwa pia na kipindi cha SHILAWADU Rais alisema kuwa
anavutiwa sana na jinsi wanavyoigiza kipindi chao
No comments:
Write comments