Mfanyabiashara
wa vinywaji mkoani hapa Festo Msalia amejiua kwa kujipiga risasi
kichwani usiku wa kuamkia jana kwa kile kinachodaiwa ni baada ya
kukamatwa na shehena kubwa ya viroba.
Kamanda
wa polisi mkoani hapa, Lazaro Mambosasa amethibitisha kutokea kwa tukio
hilo na kwamba Msalia alifariki juzi saa 5.00 usiku katika Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Dodoma
Amesema
marehemu aliondoka nyumbani kwake kwa kutumia gari aina ya Prado na
kwenda kujipiga risasi katika eneo la Veyula nje kidogo ya mji wa
Dodoma.
“Tulipata taarifa ya kujipiga
risasi juzi saa 3.00 na polisi walipokwenda waliokota maganda matano
katika eneo la tukio na walipompeleka hospitali hawakuweza kuokoa maisha
yake kwa sababu alikuwa amejichana chana na risasi, “amesema.
Alipoulizwa
kama kifo hicho kunatokana na sakata la ukamataji wa viroba, Mambosasa
amesema anafikiri suala hilo ni hisia tu kwasababu marehemu alikamatwa
Machi 3 mwaka huu akiwa na shehena ya tani 1.5 za pombe ya viroba
No comments:
Write comments