Saturday 25 March 2017

Mwanafunzi azidiwa na kukimbizwa hospitali baada ya mwalimu kumchapa viboko 10




Mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya msingi madeke halmashauri ya wilaya ya njombe mwenye umri wa miaka 10 inadaiwa kuwa anaendelea kuugulia maumivu ya adhabu ya kuchapwa viboko visivyopungua 10 na mwalimu wake wa hesabu baada ya kufeli somo hilo hapo machi 21 mwaka huu

Kwa mujibu wa baba mzazi wa mtoto huyo Bonface Manga Kwa masharti ya kutorekodiwa na waandishi mwanae Hosea Manga alichapwa viboko kumi na mwalimu wake na kisha akazidiwa na kukimbizwa hospitali.

Kutoka hospitali ya teule ya Mkoa wa Njombe Kibena ambako mtoto huyo amelazwa hali yake bado ingali si nzuri kwa kuwa hawezi kusimama wala kutembea licha ya kaimu mganga mfawidhi Wa hospitali hiyo Isaya mvinge kueleza kuwa uchunguzi wa kitabibu bado unaendelea

Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe Kupitia Mkurugenzi Mtendaji monica kwiluvya anakiri kupokea taarifa kwa njia ya simu kutoka kwa afisa elimu kata kuwa mwalimu aliyehusika anashikiliwa na polisi

Jitihada za kupata taarifa ya jeshi la polisi zimegonga mwamba baada a kamanda wa jeshi la polisi kueleza kuwa yuko nje ya mkoa kikazi.

No comments:
Write comments