Wafanyabiashara 13 wa Wilaya za
Babati na Hanang’ Mkoani Manyara, wamesalimisha katoni 1,540 za pombe
zilizofungashwa kwenye karatasi (viroba) zenye thamani ya sh140 milioni.
Wafanyabiashara hao walisalimisha katoni
hizo za pombe za viroba kabla ya upekuzi ulioendeshwa na polisi, maofisa
wa usalama wa Taifa, chakula na dawa (TFDA) na mamlaka ya mapato nchini
(TRA).
Akizungumza jana na waandishi wa habari,
kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, kamishna msaidizi (ACP) Francis
Massawe alisema wafanyabiashara hao walisalimisha wenyewe viroba hivyo
bila kushurutishwa.
Kamanda Massawe alisema katika wilaya ya Hanang’ zilisalimishwa katoni
871 na kwa wilaya ya Babati zilisalimishwa katoni 669 na wafanyabiashara
hao wanaopaswa kupongezwa kwa hatua hiyo
No comments:
Write comments