Saturday 24 June 2017

HAYA NDIYO YALIYOJIRI JANGWANI BAADA YA NIONZIMA KUTIMKA



Katibu wa Baraza la Wazee la Yanga, Ibrahim Akilimali, amesema hawana wasiwasi wowote juu ya kuondoka kwa kiungo wao Haruna Niyonzima aliyeenda Simba kwani huko nyuma wachezaji kibao waliondoka katika timu yao akiwemo Sunday Manara ‘Computer’ na timu iliendelea kufanya vizuri.
Niyonzima ameamua kuachana na Yanga kutokana na kushindwana dau la usajili kwani Simba imemtengea dola 70,000 sawa na Sh milioni 154.8 na mshahara wa dola 3,000 sawa na Sh milioni 6.6.

Akilimali amesema Niyonzima aondoke tu Yanga bila wasiwasi wowote kwani ana uhakika atapatikana mchezaji wa kuziba nafasi yake na timu itafanya vizuri.

“Mwache aende tu, Yanga ni timu kubwa na walipita wachezaji wengi zaidi yake kama vile ‘computer’ na wengine wengi ambao walikuwa wazuri lakini timu iliendelea kubaki na kufanya vizuri.


“Mwache aende huko alikoenda mchezaji asiye na hisani, Yanga kwanza mchezaji baadaye,” alisema Akilimali.

No comments:
Write comments